ABN Newletter

Mifano ya kurasa zilizotumiwa

Muhtasari

Muungano wa Bioanuai wa Afrika (ABN) inapeana mtazamo wa kipekee wa Kiafrika wa uendelevu na jamii imara, iliyojikita katika mifanyiko ya kitamaduni kupitia maeneo yake makuu ya programu. Kauli ni kuwa utofauti wa kiutamaduni na ekolojia umeunganishwa kwa ustadi na kuwa kupitia tu kwa kufufua utangamano mkubwa wa watu na ulimwengu na viumbe viishivyo humo ndipo watu wa Afrika watapata njia za kuimarisha ustawi na kuendeleza mazingira yenye afya.

Ni kutokana na hili ambapo toleo la jarida hili linajikita. Kuelewa kuwa utamaduni ndio unaunganisha maeneo yote ya ABN- maarifa ya mbegu ya jamii, usimamizi wa ekolojia ya jamii, utamaduni wa vijana na bioanuai – jarida hili linaangazia hadithi muhimu kutoka kwa washirika wa ABN kuimiza uimarishaji wa tamaduni za Afrika mahali ambapo utamaduni wa kimagharibi unabidhaisha kila kitu.

Jarida hili la kwanza lilikuwa mfululizo wa jarida zilizochapishwa ziwe za muungano huo.

Mchango wetu

Uhariri
Kuhariri kiundani
Kusoma kwa prufu

Picha
Kutafuta picha za kutumiwa kwa chapisho

Usanifu
Kutengeneza muundo wa jarida la habari
Usanifu wa picha

Uchapishaji
Nakala zilizoundwa tayari kwa uchapaji
Nakala ndogo za kusambaza mtandaoni kwa urahisi

Mwaka wa uchapishaji: 2015

Lengo la Malengo ya Maendeleo Endelevu linalohusiana na chapisho